RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MAPEPO YAKIONA CHA MOTO KATIKA MKUTANO WA INJILI ULIOANDALIWA NA NABII DANIEL SHILLAH KATIKA VIWANJA VYA AZIZI ALLY-TEMEKE DAR

Wakazi wa Temeke na dar es Salaam wanazidi kupokea maajabu ya Mungu katika mkutano mkubwa katika viwanja vya Kwa Azizi Ally Temeke jijini Dar es Salaam. Watu wanazidi kuokoka na kumpokea Bwana wetu Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yao. Ipo nguvu ndani ya mtumishi wa Mungu Nabii Daniel daniel Shillah wa huduma ya Bethel Int'l Ministry iliyopo katika jengo la IPP katika viwanja bvya maonyesho Sabasaba jijini Dar es Salaam, kupitia maombezi yake watu wanafunguliwa katika mateso ya majini, mapepo, kukosa waume/wake wa kuoa, kukosa ada, laana, umaskini, uzinzi, umbeya, majivuno, uongo, kukata tamaa, kukosa hamu ya kusoma Neno la Mungu, kushindwa mitaani, kukosa promosheni, kukosa safari za nje na mengine Mungu.

Mkutano huu utahitimishwa siku ya Jumamosi 31.12.2016 kwahiyo unaomuda wa kuhudhuria mkutano huu utakaobadilisha historia ya maisha yako ukiamini na kutii sauti ya Mungu kupitia watumishi wake. 

Mkutano umehudhuriwa na wachungaji mbalimbali kama Masanja Mkandamizaji, Mch. Advocate Addo Novemba, Smart Boy, Atosha Kissava na wengine wengi. Ikiwa ni siku ya tatu watu wanazidi kumiminika katika mkutano huu, kwani wengi wao wanapashana habari kuhusiana na matendo makuu ya Mungu yanayotokea katika viwanja vya mkutano.

Mungu akupe kibali, na shetani ashindwe kukuzuia kufika katika mkutano huu wa aina yake.
kutoka kushoto waliokaa ni Smart Boy, Nabii Daniel Shillah, Mke wa Masanja aliyesimama, Masanja Mkandamizaji aliyeshika mic wakiwa kazini kumtumikia Mungu





 MC. Joshua Makondeko