RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

01.01.2017: WATU MBALIMBALI WAINGIA KATIKA KISIMA CHA BETSAIDA KATIKA MKESHA WA CROSSOVER MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"

Baada ya kuukaribisha mwaka wa Kukumbukwa na Bwana siku ya Jumapili 01.10.2017 ambapo watu kutoka maeneo mbalimbali walikesha katika mkesha wa Crossover, Bishop Dr. Gertrude Rwakatare aliongoza msafari wa watu usiku wa kuamkia mwaka mpya 2017 hadi kwenye kisima cha Betsaida kilichokuwepo hapo kanisani Mlima wa Moto Mikocheni “B”. Wau waliweza kutumbukia katika kisima hicho huku wakiomba na kuacha shida zao katika kisima hicho kilichoombewa na watumishi wa Mungu. Kupitia kisima hicho watu waliweza kutokwa na mapepo na wengine kupokea nguvu mpya. 

Mungu ameweza kufanya mambo makubwa kwa watu waliobahatika kupita katika Kisima cha Betsaida kwa kipindi cha nyuma. Kuna shuhuda mbalimbali za watu wakishuhudia jinsi Mungu anavyobadilisha maisha yao mara tu walipokanyaga maji ya Betsaida. Kupitia kisma hicho watu wamekuawa wakiacha mikosi, balaa, nuksi, roho kama za kukataliwa, kutoolewa au kuoa, kukosa kazi, kuksa kibali, kukosa promosheni kazini, kukosa ada ya shule, kukosa kodi ya nyumba, madeni, kukosa wateja, uzinzi, umalaya, uongo, usengenyaji, utapeli, wizi, majivuno, tamaa n.k. Na siku ya mwaka mpya kuna baadhi ya watu watakuja kushuhudia jinsi Bwana analivyoweza kubadilisha historia ya maisha yao. 
Tunakukaribisha na wewe katika ibada za Mlima wa Moto Mikocheni “B” siku ya Jumapili ibada zetu zinaanza saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana na siku za katikati ya wiki ni saa 9 mchana hadi saa 1 jioni isipokuwa Jumamosi hatuna ibada. Usafiri ni bure kuanzia nje kidogo ya kituo cha mabasi cha Makumbusho jijini Dar es Salaam au Mwenge kwenye mataa, utaona magari ya Mlima wa Moto Mikocheni “B” au utasikia watu wakisema kanisania kwa mama Gertrude Rwakatare, ingia humo