RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

08.01.2017: BAADHI YA WATU WALIOKOKA SIKU YA JUMAPILI KATIKA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"

Katika ibada ya kukabidhi Malengo na Mipango ya mwaka 2017 na ugawaji wa daftari na kalamu kwa wanafunzi siku ya Jumapili 08.01.2017 katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B", watu waliweza kujitokeza kwaajili ya kuokoka. Mch. Francis Machichi na Mch. Elizabeth Lucas waliweza kuwaongoza sala ya toba na kuwaombea. Baada ya ibada kumalizika walipelekwa baharini kubatizwa kwa maji mengi. Siku ya Jumanne walianza masomo ya kukulia wokovu.

Tunakualika na wewe katika ibada ya Jumapili saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana na katikati ya wiki ibada itaanza saa 9 mchana hadi saa 1 jioni. Siku ya Jumapili usafiri ni bure kuanzia kituo cha mabasi cha Makumbusho jijini dar es Salaam au Mwenge kwenye mataa, utaona magari ya Mlima wa Moto au utasikia watu wakisema, kwa mama Gertrude Rwakatare.

Mch. Francis Machichi