Maalim Seif alijiondoa kwenye mazungumzo hayo ya maridhiano baada ya kufanyika kwa takribani vikao kadhaa, huku wajumbe wake wakiwa pamoja na marais wastaafu Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa, Dk. Salmin Amour Juma, Amani Abeid Karume na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi.
Akizungumza Rais Shein kwenye mahojiano hayo amesema …….>>>mazungumzo kweli tumefanya yalianza vizuri, yeye hakutaka kurudia uchaguzi, mimi nikasema tume imetangaza sio mimi, nikasema tume ikitangaza kuwa turudie mimi na chama changu tutakubali, lakini yeye akakataa’