Wananchi wakimuaga marehemu, Janeth Francis Songo alikuwa mwalimu wa Shule ya Msingi Maluga iliyopo Wilaya ya lramba mkoani Singida.
Stori: Dustan Shekidele, Risasi Mchanganyiko, Jan 4-6, 2017, Toleo 1388
MOROGORO: Ni majonzi makubwa! Mwalimu wa Shule ya Msingi Maluga iliyopo Wilaya ya lramba mkoani Singida, Janeth Francis Songo, wiki iliyopita alileta simanzi kubwa kwa wakazi wa mjini Morogoro baada ya kufariki katika ajali ya gari iliyosababisha vifo vya watu wawili.