RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

30.04.2017: MAMIA YA WATU WAOKOKA KATIKA IBADA YA TAMASHA LA MAOMBI MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B" SIKU YA JUMAPILI

Siku ya Jumapili 30.04.2017 ya TAMASHA LA MAOMBI lililofanyika katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B" jijini Dar es Salaam, watu wengi sana walijitokeza madhabahuni kwaajili ya KUOKOKA. Maombezi ya kuombea waliokoka yaliongozwa na Mch. Rosemary Mgetha akishirikiana na wachungaji mbalimbali wa kanisa hilo. Baada ya kuombewa na kuongozwa sala ya toba waliweza kubatizwa kwa maji mengi. Siku ya Jumanne walinanza masomo ya kukulia wokovu hapo kanisani. Tunamuomba Mungu azidi kuwapigania na kuwaimarisha katika safari yao ya WOKOVU.