RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MCH. NOAH LUKUMAY: AMINI KUPITIA TUNDA UTASA WA MAISHA YAKO UTAONDOKA NA MAISHA YAKO YATAZAA MATUNDA



"Mungu wetu ni Mungu wa upendo" Ni Mungu anayeweza kumponya mtu yeyote yule bila gharama yoyote, ni Mungu wa huruma na upendo, ni Mungu anayeweza kutumia kitu chochote kwa wakati wowote kumpa mtu muujiza wake, ni Mungu anayeweza kumtumia mtumishi wake kwaajili yako.

Je, unamini Jumapili 04.06.2017 atakuondolea shida zako katika ibada ya maombi ya kuvunja UTASA wa biashara yako, kazi yako, familia yako, ndoa yako, mahusiano yako, kibali chako, elimu yako, mifugo yako, afya yako na mambo mengi yanayokuzunguka?

Je unaamini kupitia TUNDA utakalokuja nalo Mlima wa Moto Mikocheni "B" saa 3 asubuhi, Yesu atalitumia kubadilisha HISTORIA YA MAISHA YAKO na kuwa ya baraka.

Kama unaamini, basi usikose katika ibada hii ya tofauti kabisa, uje na TUNA lako lolote lile. TUTAKUWA NA MASAA 6 IBADANI ya kufanya maombi ya hatari ya kuvunja UTASA wa maisha yako.

Usafiri ni bure kwenda kanisani na kurudi kuanzia kituo cha mabasi cha Makumbusho au Mwenge kwenye mataa barabara ya Coca Cola, utasikia watu wakisema kanisa kwa mama Rwakatare...

//Mch. Noah Lukumay//
//Mlima wa Moto Mikocheni "B"//