RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MCH. NOAH LUKUMAY: MUAMINI MUNGU TU UTAONA BARAKA ZAKE. USIKOSE IBADA YA JUMAPILI HII KUJA NA TUNDA LAKO LOLOTE LIE

Muamini Mungu TU..utaona mkono wake juu yako. Mungu wetu ni mwema na amejaa na upendo..Mungu wetu tukimwamini na kumtumia katika maisha yetu tutaona maajabu katika maisha yetu

Hakikisha kila unalofanya unamtanguliza huyu Mungu wetu, na ukifanya hivyo utaona UTASA katika maisha yako unaondoka na unakuwa ni mtu wa MAFANIKIO.

Amini watumishi wake kwani hap ndio aliowachagua kwa kazi yake kama MABALOZI hapa duniani.

JUMAPILI hii 04.06.2017 NJOO na tunda lako lolote katika ibada ya MAOMBI YA KUVUNJA UTASA katika maisha yako. Ibada itaanza saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana. Hii ni kwa wale wanaotaka maisha yao yabadilike na kuwa na maisha ya amani kuanzia afya zao, maendeleo yao, mipango yao, fikra zao, mawazo yenye majibu chanya na kila kitu wanachokitaka. Mungu akubariki..Amen

//Mch. Noah Lukumay//
//Mlima wa Moto Mikocheni "B"//
//USIKOSE KUJA NYUMBANI MWA BWANA//