RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

11.06.2017: FUNNY MGILLA NA MHE. BISHOP DR. GERTRUDE RWAKATARE WAGUSA MIOYO YA WANANDOA WASIO NA WATOTO

Muumini wa kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni “B” Funny Mgilla ambaye kwa muda mrefu ameishi maisha ya mateso kwa kukosa mtoto lakini baada ya kuombewa na Mhe. Bishop Dr. Gertrude Rwakatare aliweza kupata watoto wawili. Siku ya Jumapili 11.06.2017 Funny Mgilla aliguswa sana na somo la UTASA WA KUZAA lilohubiriwa na Bishop Dr. G. Rwakatare na ndipo alipoamua kutoa Tshs. 200,000 kama sadaka kwaajili ya wanandoa wasio na watoto ambao aliwataja kwa majina akiwemo Mr. Mbawala na mke wake. Kitendo hicho kiligusa mioyo ya watu na kujikuta watu wakilia kwasababu wanajua uchungu wa kutokuwa na watoto hasa kwa wanandoa. Baada waliombewa na Mh. Bishop Dr. G. Rwakatare pamoja na kanisa zima la Mlima wa Moto Mikocheni  “B”