RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MAAJABU: JEFF BEZOS AMZIDI UTAJIRI BILL GATES KWA SAA NNE PEKEE

Jeff Bezos.

Tajiri Jeff Bezos ameshikilia nafasi ya kwanza kwa utajiri duniani kwa saa nne na baadaye kushuka hadi ya pili.

Bezos anayemiliki mtandao wa Amazon, utajiri wake ulipanda na kufikia Dola 92.3 bilioni za Marekani akimshinda Bill Gates mwenye utajiri wa Dola 90.8 bilioni.
Bill Gates.

Tajiri Bezos alishika nafasi ya kwanza Alhamisi, Julai 27 baada ya mauzo ya hisa ya kampuni ya Amazon kupanda kwa asilimia tatu.

Hata hivyo, alishuka hadi nafasi ya pili baada ya mauzo ya hisa ya kampuni hiyo kushuka na kufikia asilimia 0.7.

Hatua hiyo ilimfanya kushika nafasi ya pili kwa utajiri wa Dola 89.3 bilioni na Gates akiwa na Dola 90.7 bilioni.

Comments