RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

Watu wenye silaha wameshambulia nyumba ya Makamu wa Rais wa Kenya


Stori iliyonifikia kutoka Kenya ni kwamba watu wenye silaha wamevamia na kushambulia nyumba ya Naibu Rais wa Kenya, William Ruto katika tukio lililotokea leo July 29, 2017.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Kenya ni kuwa watu hao walivamia nyumba hiyo na kufanya shambuli lakini muhusika ambaye ni Makamu wa Rais Ruto hakuwepo nyumbani hapo akiondoka saa moja kabla ya tukio kuungana na Rais Kenyatta kwenye mkutano wa kisiasa.

Watu wa Usalama walipofika eneo la tukio wakiwa na vifaa vya kupambana na Ugaidi kujaribu kupambana na watu katika nyumba anayoishi Ruto na familia yake ambapo hadi sasa haijafahamika waliobaki ndani wangali salama.

Comments