RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

20.08.2017: WATU WALIVYOMUABUDU MUNGU KATIKA KIPINDI CHA KUABUDU KILICHOFANYIKA KATIKA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"

Leo nataka nikupe FAIDA chache za kumwabudu Mungu wetu wa mbinguni
Kumwabudu Mungu kwamaanisha nini, na kwa nini tunapaswa kumwabudu?
Tunapowasiliana na Mungu, hatumsikilizi na kuzungumza naye kama tunavyozungumza na rafiki au mtu wetu wa ukoo. Kwa kweli, tunamwabudu Mungu na kumpa staha yenye kicho ambayo anastahili kabisa. Maisha yetu yote yanaongozwa na ibada ya kweli. Kwa njia hiyo tunaonyesha kwamba tunampenda Mungu na tunamtumikia kwa nafsi yetu yote. Ibada ya kweli inawaunganisha viumbe wote wa Mungu ambao ni waaminifu, ama mbinguni au duniani. Katika ono, mtume Yohana alimsikia malaika akitangaza amri hii: “Mwabuduni Yeye aliyezifanya mbingu na dunia na bahari na mabubujiko ya maji.”—Ufunuo 14:7.


Kwa nini tumwabudu Mungu?  Hebu fikiria sifa ambazo tumezungumzia, kama vile utakatifu, nguvu, kujidhibiti, haki, ujasiri, rehema, hekima, unyenyekevu, upendo, huruma, uaminifu-mshikamanifu, na wema. Tumeona kwamba Mungu ndiye mfano bora kabisa, na hana kifani katika kuonyesha kila sifa inayopendeza. Tunapojaribu kuelewa sifa zote za Mungu, tunatambua kwamba yeye ni mkuu zaidi, anastahili sifa zote, ni mtukufu ajabu, na yuko juu sana kuliko sisi. (Isaya 55:9) Hapana shaka kwamba Yehova ana haki ya kuwa Mwenye Enzi Kuu, naye anastahili ibada yetu. Lakini tunapaswa kumwabuduje?


Tunawezaje kumwabudu Mungu kwa roho na kweli,” na mikutano ya Kikristo hutupatia fursa ya kufanya nini?

Yesu alisema: “Mungu ni Roho, na wale wanaomwabudu yeye lazima waabudu kwa roho na kweli.” (Yohana 4:24) Ili tumwabudu Mungu “kwa roho” ni lazima tuwe na roho ya Mungu na ituongoze. Pia, ibada yetu inapaswa kupatana na kweli na ujuzi sahihi ulio katika Neno la Mungu. Tunapokutana na waabudu wenzetu, tunapata fursa ya kumwabudu Yehova “kwa roho na kweli.” (Waebrania 10:24, 25) Tunaonyesha kwamba tunampenda Mungu katika ibada safi tunapomsifu kwa nyimbo, tunaposali kwake kwa umoja, tunaposikiliza na kushiriki mazungumzo ya Neno lake.

Tunamshukuru Mungu siku ya Jumapili 20.08.2017 watu walimwabudu Mungu kwa Roho ya kweli katika ibada ya KUFUNGUA MILANGO ILIYOFUNGWA NA MAADUI ZET ILI TUSIFANIKIWE KIMAISHA iliyofanyika katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B". Kipindi cha kuabudu kiliongozwa na Roho Mtakatifu kupitia watumishi wa Mungu wanaoimba katika "PRAISE & WORSHIP TEAM ya Mlima wa Moto Mikocheni "B". Watu walionekana kuguswa na uwepo wa Mungu, Nguvu za Mungu na wakipokea Roho Mtakatifu.

Ibada hii itafanyika tena Jumapili hii saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana kwahiyo usikose kabisa. Usafiri ni bure kuanzia kituo cha Mabasi cha Makumbusho au Mwenge kwenye mataa, na baada ya ibada kuisha utarudishwa kituoni. Mungu akubariki sana.

Furaha Isaya

Mh. Bishop Dr. Gertrude Rwakatare akiombewa





























Comments