RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

Mahakama yavunja ndoa India kisa Choo


Mahakama moja ya India imetoa ruhusa kwa mwanamke mmoja nchini humo kupewa talaka baada ya kufungua kesi akilalamikia kitendo cha mume wake kutojenga choo nyumbani kwao.

Wawili hao walifunga ndoa miaka mitano lakini kitu cha ajabu ni mwanaume kutojenga choo kitu ambacho kilimfanya mwanamke huyo kusubiri nyakati za usiku ndipo aweze kujisaidia vichakani jambo ambalo alilodai kuwa ni ukatili na hudhalilisha utu wa wanawake.

Jaji wa Mahakama hiyo alisema>>>”Watu wanatumia pesa nyingi kwa ajili ya starehe kwenye kununua sigara, pombe, simu za mkononi na vitu vingine lakini wanashindwa kujenga vyoo kwa ajili ya familia zao, huu ni ukatili.”

Comments