RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MAAFALI YA DARASA LA SABA SHULE YA KIHONDA ST. MARY'S MOROGORO YAFANYIKA KWA KISHINDO

Tunawapongeza wanafunzi wa darasa la saba kwa kufanya maafali katika shule bora Tanzania ya Morogoro Kihonda St Mary's kwa mwaka 2017. Pia tunampongeza Mh. Bishop Dr. Gertrude Rwakatare Rwakatare na MD. Rose Rwakatare kwa jitihada zao za kuhakikisha shule inapata walimu bora, masomo bora, vyakula vya kutosha, vitabu vya kutosha, wafanyakazi wenye kujituma., maktaba nzuri, viwanja vya michezo, maabala nzuri. Shule imekuwa ni moja ya shule bora Tanzania kwa kufaulisha na maadili mema kuanzia walimu, wafanyakazi na wanafunzi. Mazingira yanaruhusu mwananfunzi kujisomea na kufanya michezo mbalimbali inayopatikana katika shule hiyo.

Watu wengi wanajiunga na shule hii kutokana na historia nzuri ya kitaaluma na kimaadili. Wanafunzi mara nyingi wanapata muda mwingi wa kujisomea na kukaa na walimu wao baada ya masomo ili kuweza kuwaauliza pale ambapo hawakuelewa vyema. Shule hii imebahatika kuwa na maktaba nzuri yenye vifaa vyote vya wanafunzi kujifunzia na pia maktaba yenye vitabu vyakutosha vya kujisomea.

Pengine ulikuwa unahangaika na shule ya kuwapeleka watoto wako ili wapate elimu bora na maadili mema kutoka kwa walimu, sasa mkombozi wako amekufikia, wapeleke wanao Kihonda St. Mary's Morogoro ili wapate elimu bora na maadili mema.
 MD. Rose Rwakatare akiongea na mwananfunzi












Comments