RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

24.12.2017: BAADHI YA WATU WALIOKOKA SIKU YA MAANDALIZI YA MKESHA WA KRISMASI KATIKA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"

Hawa ni baadhi tu ya watu waliokoka katika maandalizi ya mkesha wa mwaka mpya siku ya Jumapili 24.12.2017 katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B" linaloongozwa na Mhe. Bishop Dr. Gertrude Rwakatare. Mchungaji Manumbu aliwaongoza sala ya toba na baadae wachungaji wa kanisa hilo waliwaombea na kuwatamkia baraka.

Wewe ambaye hujaokoka, Mungu anakupenda, ni muda wako sasa wa kuamua kumtumikia Mungu. Amua sasa kuokoka. Tunakukaribisha katika ibada ya Jumapili hii Mlima wa Moto Mikocheni "B". Ibada itaanza saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana. Utaweza kupata muda mzuri wa kuongozwa sala ya toba na baadae kubatizwa kwa maji mengi.

Kanisa limeaandaa usafiri wa bure wa kufika kanisani kuanzia kituo cha mabasi cha Makumbusho na Mwenge kwenye mataa barabara ya Coca Cola.



Mch. Manumbu
























Comments