RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

21.01.2018: MCH. PRSICA CHARLES ALIVYOONGOZA KIPINDI CHA KUSIFU NA KUABUDU KATIKA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI “B”

Hivi ndivyo waumini wa kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B" walimvymuabudu Mungu na kupeleka maombi yao mbele za Mungu siku ya Jumapili 21.01.2018. Ilikuwa ni ibada iliyojaa upako na nguvu za Mungu. Watu waliguswa na nguvu za Mungu wakati wakiimba nyimbo za kuabudu wakiongozwa na Mch. Prisca Charles pamoja na Praise and Worship Team ya kanisani hapo. Ilikuwa ni ibada iliyojaa uwepo wa Mungu.

Kwako wewe ambaye ulikosa ibada hii, tunakualika katika ibada ya Jumapili hii itakayoanza saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana. Ni siku yako ya kufunguliwa katika shida zako na kuomba ulinzi kutoka kwa Mungu katika maisha yako pamoja na familia yako. Wapowatu wengi sana walikuja hapa kanisani wakiwa na shida mbalimbali kama kuoa/kuolewa, kuapata kazi, kuponya, kuinuliwa imani zao, kuinuliwa huduma zao, kupata kibali, kupata mafanikio, kufarijiwa, kupata watoto, kuapa wateja, kujenga, kununua viwanja, kuanza miradi mbalimbali n.k, Mungu aliweza kuwatimizia. Pengine na wewe ungetamini Mungu kutumiza malengo yako ya mwaka kwa kishindo! Tunakualika katika ibada hii. Njoo ukiwa na imani ya kupokea, ondoa hofu na kuona haitawezekana..Uwe Mutu wa imani.

Kanisa limeandaa usafiri wa bure kuanzia kituo cha mabasi cha Makumbusho na Mwenge kwenye mataa barabara ya Coca Cola jijini dar es Salaam, Tanzania. Karibuni sana


Mch. Prisca Charles
























Comments