RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

TANZIA: MAMA YAKE LADY JAYDEE AFARIKI DUNIA


MAMA mzazi wa msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’, Bi. Martha Mbibo, amefariki dunia alfajiri ya leo Alhamisi Aprili 26, 2018.

Kaka wa Lady Jaydee ambaye pia ni msanii Dabo, amethibitisha taarifa hizo na amesema kwamba mama yao amefariki akiwa nyumbani kwake baada ya kuugua Saratani kwa muda mrefu.

Dabo amesema msiba upo nyumbani kwa marehemu Jet jijini Dar es salaam ambapo familia ya marehemu itatoa utaratibu wa mazishi mara baada ya utaratibu wa kuupeleka mwili hospitali kuhifadhiwa kukamilika.

Comments